Makamu wa Rais wa Tanzania amekiambia kikao cha 77 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa nchi yake iko tayari kutuma wanajeshi wake popote ulimwenguni kwa ajili ya kulinda amani chini ya mpangilio wa UN.
Rais wa Marekani Joe Biden amelihutubia Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Jumatano, akiwa na msimamo thabiti dhidi ya uvamizi wa Russia nchini Ukraine na tishio la Russia kutumia silaha za nyuklia. Pia amezungumzia kuhusu chakula, hali ya hewa, na masuala mengine nyeti.
Rais wa Marekani Joe Biden amepangwa kuhutubia baraza kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York Jumatano wakati akitarajia kuangazia juhudi za utawala wake katika kukabiliana na ukosefu wa usalama wa chakula ulimwenguni, kati ya masuala mengine.
Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa umefunguliwa rasmi Jumanne kwa mkuu wa umoja huo kutoa onyo kali kuhusu "msimu ujao wa baridi wenye malalamiko kote dunaini kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa, kupanda kwa bei za bidhaa pamoja na mizozo inayosababisha mauaji mengi.
Umoja wa Mataifa umelaani kifo cha Mahsa Amini kilichotokea alipokuwa anashikiliwa na polisi wa Tehran, nchini Iran.
Usikose kufuatilia habari na vipindi maalum katika lugha 16 tofauti kuhusu kongamano la viongozi moja kwa moja kutoka makao makuu ya Umoja wa Mataifa New York na Washington DC, tutakuarifu kila tukio...
Mkutano mkuu wa kila mwaka wa viongozi kwenye Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UNGA) unaanza wiki ijayo ukigubikwa na mazishi ya Malkia Elizabeth na wakati vita vya Ukraine vikielekea kuingia katika kipindi ambacho kinaweza kuwa muhimu sana.
Kila Septemba, viongozi kutoka kote duniani wanafika makao makuu ya Umoja wa Mataifa kwa ajili ya majadiliano ya kila mwaka kwenye Baraza Kuu. Lakini basi nini UNGA na kipi ni muhimu sana kuhusu mjadala huu wa kila mwaka?
Kiongozi wa chama cha Ford Kenya, Moses Wetangula, amechaguliwa kuwa spika wa bunge la taifa la Kenya.
Rais mteule wa Kenya William Ruto aliahidi mambo mengi wakati wa kampeni, alipokuwa akitafuta kura kuelekea ikulu.
Ndoto ya Raila Odinga, mtoto wa makamu wa rais wa Kwanza wa Kenya Jaramogi Odinga, kuwa rais wa Jamhuri ya Kenya imeonekana kuzima kabisa hii leo, baada ya mahakama ya juu kuidhinisha ushindi wa Dr. William Ruto.
Pandisha zaidi