Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Antony Blinken aliwasili Mashariki ya Kati leo Jumapili, akianza ziara ya siku tatu huku ghasia zikipamba moto kati ya Waisraeli na Wapalestina, na huku Iran na vita vya Ukraine vikiwa katika ajenda ya juu.
Televisheni ya taifa nchini Libya imesema Waziri Mkuu huyo wa Italia alipokelewa na Abdelhamid Dbeibah ambaye anaongoza serikali ya umoja wa kitaifa yenye makao yake mjini Tripoli ambayo inazozaniwa na utawala hasimu wa mashariki mwa nchi hiyo
Katika mkutano ulioongozwa na Waziri Mkuu Li Keqiang, baraza la serikali ya China ambalo linafanya kazi kama baraza la mawaziri liliapa kuharakisha utoaji wa miradi ya uwekezaji wa kigeni, kuendeleza uthabiti wa sarafu ya China ya Yuan, kurahisisha usafiri katika mipaka ndani na nje ya nchi
Shambulio la Jumamosi linakuja chini ya saa 24 baada ya watu saba kuuawa kwa kupigwa risasi na mpalestina aliyekuwa bunduki katika sinagogi kwenye viunga vya Jerusalem. Watu 10 walijeruhiwa katika shambulio la Ijumaa kabla ya polisi kuwasili na kumuua mtu huyo mwenye silaha
Katika taarifa iliyoonekana na shirika la habari la AFP siku ya Jumamosi, CMA ilielezea hilo pamoja na makundi mengine yote yenye silaha yaliotia saini makubaliano ya amani mwezi Desemba yalisitisha ushiriki katika mchakato wa amani kwa sababu ya "ukosefu wa nia ya kisiasa katika kuutetea"
Wizara ya Uingereza imesema wizara ya Russia "huenda ilifanya tathmini" kuwa haiwezi kuepuka kuzungumzia shambulio hilo kwa sababu makamanda wa Russia wamekuwa wakikosolewa vikali kufuatia tukio hilo
Jeshi la anga limesema mmoja wa marubani kati ya watatu waliohusika katika ajali hiyo ya jumamosi asubuhi amefariki dunia
Balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa, Linda Thomas Greenfield anasema juhudi kubwa zinahitajika nchini Msumbiji kuwasukuma waasi ambao wasambaa kusini kutoka kaskazini katika jimbo la Cabo Delgado.
Wakati Makamu wa Rais w zamani wa Marekani Mike Pence amejiunga na kundi la maafisa wa ngazi ya juu waliokiuka utunzaji wa nyaraka za siri.
Ripoti ya taasisi yake iliyataja mapinduzi nane yaliyofanikiwa tangu mwaka 2019. Mali na nchi jirani ya Burkina Faso zimeshuhudia mawili kila moja katika kipindi hicho na kuyumbisha zaidi sehemu ya dunia ambayo tayari imezingirwa na wanamgambo wa Kiislamu
Rais wa zamani wa Kenya, Uhuru Kenyatta ni mpatanishi katika mzozo wa eneo hilo tete kwa niaba ya nchi saba wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki."Alielezea wasiwasi mkubwa juu ya hali inayozidi kuzorota" huko Kivu Kaskazini ambako mapigano yamezuka "kati ya makundi mbalimbali yenye silaha
Hatua hii imekuja kufuatia Waziri Mkuu Su Tseng-chang aliyewasilisha barua yake ya kujiuzulu wiki iliyopita pamoja na ile ya baraza lake la mawaziri kabla ya kuundwa upya kwa serikali inayotarajiwa kuwa na mabadiliko
Pandisha zaidi