Maadhimisho ya Kumbukumbu ya siku 100 za mauaji ya kimbari yakiendelea huko Kigali, Rwanda. Picha zote kwa hisani ya Ikulu ya Kigali.
Kura zinahesabiwa nchini Madagascar baada ya kufanyika kwa uchaguzi wa rais ulosusiwa na idadi kubwa ya wapinzani. Uchaguzi umefanyika baada ya wiki kadhaa za ghasia na maandamano, na katika mji mkuu wa Antananarivo wafuatiliaji wanasema uchaguzi umefanyika kwa amani.
Maafisa wa afya wa Gaza wanasema ukosefu wa mafuta imesababisha kusitishwa kazi kwenye hospitali kadha Gaza kaskazini ambako watoto watano wachanga wamefariki Jumapili pamoja na wagonjwa 7 walokua mahtuti baada ya mashini za kuwapa oxygen kusita kufanya kazi.
Wataalam wanasema Hamas imetekeleza uhalifu wa kivita kwa kufanya mashambulizi holela ya roketi na shambulizi la Oktoba 7 dhidi ya Israel ambalo lilisababisha vifo vya watu 1,400.