Rais wa Marekani, Joe Biden, amezidisha mashambulizi yake dhidi ya rais wa zamani Donald Trump, Alhamisi, katika hotuba kali ambayo amewahi kutoa hadi sasa, kwamba rais huyo wa zamani na mgombea anaeongoza katika chama cha Republikan, ni kitishio kwa desturi na taasisi za kidemokrasia za nchi.