Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken alisema Jumatano ana wasiwasi mkubwa kuhusu ripoti ya Umoja wa Mataifa inayosema Rwanda inawaunga mkono waasi katika nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Zaidi ya vituo vya kupigia kura 43,000 vimewasilisha matokeo yao ya uchaguzi wa rais kutokana na kura zilizopigwa Jumanne. Matokeo ya awali yanaonyesha ushindani mkali kati ya wagombea wawili wakuu wa uchaguzi wa urais.
Matokeo ya awali yaliyotangazwa na kituo cha televisheni cha Kenya yanaashiria kuna ushindani mkali wa kinyang’anyiro cha urais kati ya Naibu Rais William Ruto na Raila Odinga, kiongozi mkongwe wa upinzani ambaye anaungwa mkono hivi sasa na chama tawala.
Mgombea mwenza wa Muungano wa Azimio la Umoja One Kenya Martha Karua amezungumza kwa mara ya kwanza tangu kupiga kura yake katika uchaguzi wa Jumanne.
Milipuko miwili iliua wanajeshi 15 wa Burkina Faso Jumanne, jeshi limesema, likiwa shambulio la hivi karibuni katika msusuru wa mashambulizi kama hayo wakati nchi hiyo ikipambana na uasi wa wanamgambo wa kiislamu.
Marekani inasema itatoa dola milioni 89 kusaidia kutegua mabomu ya ardhini, vilipuzi na vifaa vingine ambavyo havijalipuka vilivyowekwa nchini Ukraine na wanajeshi wa Russia.
Serikali ya Guinea iliyoteuliwa na jeshi imelivunja vuguvugu la upinzani nchini humo, lijulikanalo kama National Front for the Defence of the Constitution (FNDC), chini ya amri iliyothibitishwa na shirika la habari la AFP Jumanne.
Mwenyekiti wa tume huru ya uchaguzi na mipaka ya Kenya IEBC Wafula Chebukati, amesema kwamba matokeo ya kura yaliyotangazwa kwenye vituo vya kupigia kura ndiyo ya mwisho, na kwamba hayawezi kubadilishwa na mtu yeyote.
Mbunge maarufu magharibi mwa Kenya Didmus Barasa amekamatwa kwa madai ya kumpiga risasi dereva wa mpinzani wake wakati wa zoezi la kuhesabu kura.
Wanasiasa maarufu na wa muda mrefu nchini Kenya wameanza kukubali kushindwa hata kabla ya matokeo rasmi kutangazwa.
Polisi wanamzuia afisa wa tume huru ya uchaguzi na mipaka ya Kenya IEBC kwa kuhusishwa na wizi wa kura.
Wanamgambo wameuwa wanajeshi 17 wa Mali na raia wanne katika shambulio karibu na mji wa Tessit siku ya Jumapili, jeshi la Mali lilisema.
Pandisha zaidi