Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 00:34

Kenya yaipiku Tanzania kidemokrasia - Ripoti


Rais John Pombe Magufuli
Rais John Pombe Magufuli

Tanzania imepoteza nafasi yake kama taifa lililokuwa linaongoza zaidi katika demokrasia katika eneo la Afrika Mashariki na inafahamika hivi sasa inashindana na maeneo yenye hali ya hatari kisiasa duniani, ripoti mpya imesema.

Gazeti la “The Citizen” linalochapishwa nchini Tanzania limeandika kuwa Kenya imeipiku Tanzania.

Tanzania imeshuka daraja saba kwa mwaka mmoja uliopita , na kupata jumla ya alama 45 tofauti na utafiti wa 2018 ulioipa alama 53.

Lakini Ripoti hiyo 'Freedom in the World Report 2019' iliyotolewa siku ya Ijumaa inaonyesha kwamba Kenya ndio inayoongoza kidemokrasia miongoni mwa mataifa ya Afrika mashariki.

Kenya

Maridhiano kati ya Rais Uhuru Kenyatta na kiongozi wa upinzani nchini Kenya, Raila Odinga ni yaliyoifanya Kenya kuwa katika sura tofauti ya kisiasa na ilichangia kujipatia alama 48.

Mwaka 2018 ripoti iliyotolewa ilikuwa inaonyesha Kenya imeshuka kidemokrasia.

Katika ripoti ya mwaka 2019 Burundi imechukuwa nafasi ya mwisho kama taifa lenye uhuru wa kisiasa kwa kupewa alama 18 ikifuatiwa na Rwanda yenye alama 23 na Uganda ilipata alama 37.

Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza
Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza

Tafiti hiyo inaeleza kuwa licha ya kuwa Tanzania na Kenya zina alama tofauti zote mbili ni katika mataifa yanayoorodheshwa kuwa na uhuru mdogo wa kidemokrasia.

Rais wa Uganda Yoweri Museveni
Rais wa Uganda Yoweri Museveni

Burundi, Uganda na Rwanda

Kwa mujibu wa ripoti hiyo orodha nyengine ni ya mataifa yalio 'huru' na 'yasio huru' ambapo Uganda, Burundi na Rwanda ni mataifa yasio na uhuru wa kidemokrasia.

Rais wa Rwanda Paul Kagame
Rais wa Rwanda Paul Kagame

Tanzania

Utafiti huo uliofanywa na shirika la Freedom House, umeiweka Tanzania miongoni mwa mataifa 10 yanayofuatiliwa mwenendo wake wa kidemokrasia katika mwaka 2019 .

Freedem House ni shirika huru lenye makao yake Marekani lilojikita katika kueneza uhuru na demokrasia duniani kote.

Mbali na Tanzania , mataifa mengine yanayoangazwa na shirika hilo ni Armenia, Brazil, Cambodia, Cameroon, China, Ethiopia, Iraq, Poland na Sri Lanka.

Sababu za kushuka daraja

Ripoti hiyo inaeleza sababu za kushuka daraja kwa Tanzania ni kufuatia hatua ya serikali kuwaweka ndani viongozi wa upinzani, kuzuia maandamano dhidi ya serikali na kupitisha sheria zinazokipendelea chama tawala katika siasa za ngazi za chini 2018.

Uganda ilishuka kutoka taifa lenye 'Uhuru kiasi' hadi lisilo na Uhuru kutokana na Rais Yoweri Museveni kuzuia uhuru wa kujielezea, kuvidhibiti vyombo vya mawasiliano mbali na kuidhibiti mitandao ya kijamii kwa kuweka kodi.

Rwanda imepata alama hizo kutokana na ukamataji wa viongozi wa upinzani na matishio yanayotolewa na Rais Kagame kwa vyama vya siasa.

Kadhalika ripoti inasema uongozi wa Kagame wa kidikteta umeathiri vibaya demokrasia nchini humo.

Kwa upande wa Burundi imepata alama hizo kutokana na uongozi wa Rais Pierre Nkurunziza Kuendelea kuwanyamazisha wapinzani na kukiuka katiba.

XS
SM
MD
LG