Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 17:14

Serikali ya Burundi kutoshiriki kikao cha marais wa jumuiya ya Afrika mashariki


Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza akizungumza na waandishi katika mkoa wa Ngozi, kakskazini mwa Burundi, Mei 17, 2018.
Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza akizungumza na waandishi katika mkoa wa Ngozi, kakskazini mwa Burundi, Mei 17, 2018.

Serikali ya Burundi umesema haitashiriki kikao cha marais wa jumuiya ya Afrika mashariki, awamu ya 20 mjini Arusha Tanzania kwa msingi kwamba haijafanya matayarisho kuhudhuria kikao hicho.

Barua ya rais wa Burundi Pierre Nkurunziza, kwa mwenyekiti wa jumuiya ya Afrika mashariki Yoweri Museveni, inaomba mkutano uahirishwe kwa muda wa mwezi mmoja zaidi.

Lakini Museveni, kwa kumjibu Nkurunziza, amesisitiza kwamba mkutano huo lazima ufanyike ilivyopangwa, kwa sababu maandalizi yamekamilika.

XS
SM
MD
LG