Kiongozi wa kanisa Katoliki Papa Francis, ameyataka mataifa ya nje kuacha kupora mali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na bara la Afrika kwa jumla, ili kutosheleza tamaa yao.
Ndege za kijeshi za jamhuri ya kidemokrasia ya Congo zimeendelea kushambulia waasi wa kundi la M23 wanaoshikilia mji wa Kitchanga, Kivu kaskazini, mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.
Mahakama moja ya Kenya siku ya Jumatano ilimkuta na hatia mwanadiplomasia wa Venezuela kwa kumuua kaimu balozi wa taifa hilo la Amerika Kusini muongo mmoja uliopita nyumbani kwake katika ujirani karibu na mjini Nairobi.
Serikali ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo imeonya kwamba haitaendelea kuvumilia kile imekitaja kama unyanyasaji wa jirani yake Rwanda, licha ya kutakiwa kufuata utaratibu wa kuleta amani mashariki mwa nchi hiyo na kwamba ina haki ya kujilinda na kulinda ardhi yake kwa nguvu zote.
Waziri wa zamani wa elimu wa Kenya Profesa George Magoha amefariki. Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa na gazeti la Daily Nation, mke wake Dkt Magoha amethibitisha kifo hicho.
Kinara wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga Jumatatu alisisitiza kuwa yeye ndiye mshindi halali wa uchaguzi wa mwaka jana, na kuzidisha madai ya udangayifu miezi mitano baada ya uchaguzi.
Serikali ya Rwanda imesema kwamba Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo DRC inasajili mamluki na kuvuruga mchakato wa kuleta amani nchini humo.
Tanzania imeipiga marufuku kampuni ya Kenya inayonunua maparachichi yake ikidai inajihusisha na vitendo haramu ikiwa pamoja na kuendesha biashara bila kibali.
Mastaa wa Nigeria kama vile Burna Boy, Davido na Wizkid wametawala katika orodha ya washindi kwenye tuzo za nane za All Africa Music Awards (Afrima).
Polisi wametumia gesi ya kutoa machozi kuwatawanya maandamanaji katika mji wa Goma Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, wanaotaka maafisa kuhakikisha kwamba waasi wa kundi la M23 wanaondoka sehemu hiyo.
Raia wa Kenya wana maoni mseto kuhusu utendakazi wa Tume ya Uchaguzi nchini humo, IEBC, chini ya uenyekiti wa Wafula Chebukati ambaye amemaliza utumishi wake Jumanne, hii pamoja na makamishna wengine wawili—Boya Molu na Prof Abdi Guliye—baada ya kuhudumu kwa miaka sita.
Maamuzi ya kuanzisha tasisi ya Fedha ya Afrika Mashariki – Benki Kuu ya Afrika Mashariki – yatafanyika mwaka huu wa 2023, jambo kuu linalohitajika katika utekelezaji utaratibu wa kuwa na sarafu moja.
Pandisha zaidi