Kennes Bwire is a journalist with Voice of America and is based in Washington DC.
Rais wa Uganda Yoweri Museveni amesema kwamba serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imewaruhusu wanajeshi wa Uganda UPDF, kuingia sehemu zaidi ambazo waasi wa kundi la Allied Democratic Forces ADF wanaaminika kujificha, na kuwashambulia waasi hao.
Mtoto wa rais wa Uganda Yoweri Museveni, Lt. Jenerali Muhoozi Kainerugaba, amesema kwamba kundi la waasi la M23, linalopigana vita na jeshi la serikali ya Kinshasa, lina haki ya kufanya hivyo.
Ndege yenye watu 43 imepoteza rada na kuanguka katika ziwa Victoria, karibu na uwanja wa ndege wa Bukoba nchini Tanzania.
Serikali ya Uganda imefutilia mbali ripoti kwamba inaunga mkono kundi la waasi la M23 ambao wanashikilia sehemu za mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Felix Tshisekedi amewaelekeza viongozi wa jeshi la nchi hiyo kufungua kambi kadhaa za mafunzo ya kijeshi kote nchini humo, kwa matayarisho ya kusajili idadi kubwa ya wanajeshi kupambana na kundi la waasi la M23 na makundi mengine ya waasi Kivu kaskazini.
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amekutana na rais wa China Xi Jinping mjini Beijing na kusaini mikataba mbalimbali ya ushirikiano ambayo wanadiplomasia wamesema itanufaisha kila upande.
Jeshi la Kenya KDF, linatayarisha kikosi chake kukituma mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kama sehemu ya kikosi cha Jumuiya ya Afrika Mashariki kupambana na makundi ya waasi ambayo yamepelekea kukosekana kwa amani sehemu hiyo.
Marekani imeshumu mapigano yanayoendelea Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kati ya kundi la waasi la M23 na wanajeshi wa serikali ya DRC na kuwataka waasi kuachilia sehemu wanazozishikilia na kuweka chini silaha.
Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imesema kwamba haitafanya mazungumzo na kundi la waasi la M23, ikilitaja kundi hilo ni la kigaidi.
Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo imemuita balozi wake wa Rwanda kurudi Kinshasa kwa mashauriano.
Rwanda imetuma wanajeshi kwenye mpaka wake na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, saa chache baada ya DRC kumfukuza balozi wa Rwanda kwa madai ya DRC kwamba serikali ya rais Paul Kagame inawaunga mkono waasi wa M23.
Rais wa Kenya Dr. William Ruto, amesema kwamba yupo tayari kufanya kazi na mmoja wa viogogo wa muungano wa Azimio Kalonzo Musyoka.
Mshauri wa usalama wa taifa wa rais wa Marekani Jake Sullivan, amefanya mazungumzo na mwenzake wa Kenya Dr. Monica Juma kuhusu vita vya Ethiopia na mgogoro wa kibinadamu unaoendelea kuongezeka nchini humo.
Mfuasi mkubwa wa chama kikuu cha upinzani nchini Uganda Sam Mugumya, ambaye amekuwa akizuiliwa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwa muda wa miaka 8, ameachiliwa huru.
Waziri Mkuu wa Uingereza Liz Truss amejiuzulu kama kiongozi wa chama cha Conservative.
Mshauri wa ngazi ya juu kuhusu operesheni maalum wa rais wa Uganda, Jenerali Muhoozi Kainerugaba, amesema kwamba hataacha kuandika ujumbe wenye utata kwenye mitandao ya kijamii na kwamba yeye si mtoto wa kuambiwa cha kufanya.
Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imesema haitafanya mazungumzo na kundi la waasi la M23, baada ya kundi hilo kusema kwamba lipo tayari kwa mazungumzo hayo.
Rais wa Uganda Yoweri Museveni amesaini mswaada wa matumizi ya mitandao ya kijamii na kuwa sheria na hivyo kuwaweka watumiaji wa mitandao hiyo katika hatari ya kufungwa hadi miaka 5 gerezani endapo watachapisha au kusambaza haabri ambazo zinaikera serikali au watu binafsi.
Idadi kubwa ya nchi wanachama katika Umoja wa Mataifa zimepiga kura ya kuikashifu hatua ya Russia kwa kujiingiza katika mikoa minne ya Ukraine.
Mgombea wa urais mara 5 bila mafanikio nchini Kenya Raila Odinga, ameendelea kuishutumu mahakama na tume ya uchaguzi, akidai kwamba alipokonywa ushindi katika uchaguzi mkuu wa mwezi Agosti.
Pandisha zaidi