Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Juni 17, 2025 Local time: 16:28

Kesi ya kamanda wa zamani wa waasi Jamhuri ya Afrika ya Kati yaanza ICC


Mahamat Said Abdel Kani akiwa mbele ya Mahakama Kuu ya Kimataifa ya Uhalifu huko the Hague, Uholanzi, Jumatatu, Sept. 26, 2022.
Mahamat Said Abdel Kani akiwa mbele ya Mahakama Kuu ya Kimataifa ya Uhalifu huko the Hague, Uholanzi, Jumatatu, Sept. 26, 2022.

Kamanda wa zamani wa waasi nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati amedai hana hatia Jumatatu wakati wa kuanza kesi ya uhalifu wa vita dhidi yake katika mahakama kuu ya kimataifa ya uhalifu.

Mahamat Said Abdel Kani mwenye umri wa miaka 52 anayedaiwa kuwa mwanachama wa kundi lililokuwa linaongozwa na waislamu la Seleka, anatuhumiwa kwa kuwatesa wafuasi wa upinzani wakati nchi ilipokuwa inatumbukia katika vita vya wenyewe kwa wenyewe mwaka 2013.

Wakimbizi kutoka Jamhuri ya Afrika ya Kati wakipata vitambulisho vyao vya kidijitali katika kambi ya wakimbizi ya Gado-Badzere, Cameroon. June 26, 2022.
Wakimbizi kutoka Jamhuri ya Afrika ya Kati wakipata vitambulisho vyao vya kidijitali katika kambi ya wakimbizi ya Gado-Badzere, Cameroon. June 26, 2022.

Kani anashutumiwa kumuua kiongozi wa polisi katika mji mkuu wa Bangii mwaka 2013 ambako wafuasi wa rais aliyetimuliwa Francois Bozize waliteswa vibaya.

Mwendesha mashtaka atategemea ushahidi wa watu 43 katika kesi hiyo ambayo inatarajiwa kudumu kwa miezi kadhaa.

Kundi la utetezi la la Bw Said limetoa hoja kwamba linashaka na ushahidi uliotolewa dhidi yake.

XS
SM
MD
LG