Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 15:42

Mahakama ya uhalifu wa kivita yaanza vikao Afrika ya kati


Wapiganaji wa Seleka wakitembea mitaani katika mji wa Bria, Jamhuri ya Afrika ya kati. PICHA: AP
Wapiganaji wa Seleka wakitembea mitaani katika mji wa Bria, Jamhuri ya Afrika ya kati. PICHA: AP

Mahakama maalum ya kesi za uhalifu huko jamhuri ya Afrika ya kati imeanza kusikiliza kesi ya kwanza leo Jumanne, ikiwa ni miaka saba tangu ilipoundwa.

Mahakama hiyo yenye majaji na waendesha mashtaka wa kimataifa na wa Jamhuri ya Afrika ya kati, ilianzishwa kuchunguza uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya ubinadamu uliofanyika miongo miwili iliyopita.

Vikao vya mahakama vinafanyika mjini Bangui.

Kuanzishwa kwa mahakama hiyo ni hatua ambayo imesifiwa na baadhi ya majaji wanaoheshimiwa sana na kutajwa kama hatua nzuri sana katika kuhakikisha kwamba haki inapatikana kutokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe vya miaka mingi.

Lakini baadhi ya watu wameelezea mashaka yao kuhusu utendaji wake utakavyokuwa.

Wanaoshitakiwa katika mahakama hiyo ni wanachama wa kundi la wapiganaji la 3R lenye nguvu sana katika Jamhuri ya Afrika ya kati.

Kundi hilo linashutumiwa kwa mauaji ya darzeni ya watu katika sehemu za kaskazini magharibi mwa nchi.

Rais wa mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC, Piotr Hofmanski, ameandika ujumbe wa twiter akiiunga mkono mahakama hiyo maalum

XS
SM
MD
LG