Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 17:40

Benki ya Dunia kuikopesha Kenya dola bilioni moja


Rais wa Kenya William Ruto akizungumza na waandishi wa habari katika Ikulu ya Nairobi, Terehe 2 Aprili 2023. Picha na Tony KARUMBA/AFP.
Rais wa Kenya William Ruto akizungumza na waandishi wa habari katika Ikulu ya Nairobi, Terehe 2 Aprili 2023. Picha na Tony KARUMBA/AFP.

Benki ya Dunia ilisema siku ya Jumanne imeidhinisha mkopo wa dola bilioni moja kwa Kenya ili kusaidia katika bajeti ya taifa hilo kubwa kiuchumi la Afrika Mashariki ambalo linakabiliwa na madeni makubwa na kudhoofika kwa sarafu yake.

Ukopeshaji utafanywa kupitia chombo cha mkopo kiitwacho Development Policy Operations (DPO), ambacho kitaifanya Kenya kuanzisha mageuzi yenye lengo la kufungua uwanja wa kifedha, kuboresha ushindani wa kilimo na kuboresha utawala.

"Mageuzi ya serikali, yanayoungwa mkono na DPO, yatasaidia kufanikisha uimarishaji wa sera za serikali zenye lengo la kupunguza nakisi na ulimbikizaji wa deni, kitu ambacho ni muhimu katika kupunguza mzigo wa deni na athari zinazohusiana nazo, kwa usawa na njia endelevu," alisema Mchumi Mwandamizi wa Benki ya Dunia nchini Kenya, Aghassi Mkrtchyan katika taarifa.

Rais William Ruto, ambaye alichaguliwa mwaka jana, aliahidi kurejesha nidhamu ya fedha katika serikali baada kuongezeka kwa deni la taifa wakati wa utawala wa raisi aliyemtangulia.

Lakini pendekezo lake la kuongeza kodi katika nyanja mbalimbali za kiuchumi ikiwa ni sehemu ya mswaada wa sheria ya fedha ambao serikali yake itawasilisha bungeni mwezi ujao, mswaada huo umekabiliwa na upinzani kutoka kwa watumishi wa umma na wapinzani wa kisiasa.

Kenya ilipitishwa kupata ufadhili kupitia chombo cha DPO mwaka 2019 na tangu wakati huo nchi hiyo imekuwa ikipokea mikopo kama hiyo minne, mkopo wa mwisho ulikuwa mwishoni mwa Machi.

Uchumi wa Kenya unatarajiwa kukua kwa asilimia 5.8 mwaka 2023 kutoka asilimia 4.8 mwaka 2022. Benki kuu ya nchi ilisema mwezi Machi.

Chanzo cha habari hii ni shirika la habari la Reuters.

Forum

XS
SM
MD
LG