Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio ametangaza kuwa balozi wa Afrika Kusini kwa Washington hatakiwi nchini wakati uhusiano wa nchi hizo mbili ukidorora.
Botswana imepata dola milioni 4 kutokana na mauzo ya leseni za uwindaji wanyama pori, ikiwa ni kiwango cha juu tangu kuondolewa marufuku ya uwindaji mwaka 2019.
Utafiti mpya umebaini kuwa ugonjwa wa kisukari aina ya Type 2 unaongezeka kwa kasi miongoni mwa baadhi ya watu barani Afrika Kusimi mwa Sahara kuliko ilivyodhaniwa.
Mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa yanasema visa vya ugonjwa wa surua barani Ulaya vimeongezeka maradufu ikilinganishwa na mwaka uliopita, vikiongezeka hadi 127,000, idadi ya juu sana tangu mwaka 1997.
Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia Watoto, UNICEF, Alhamisi alisema kwamba Watoto milioni 16 nchini Sudan wanateseka vibaya kutokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo.
Rais wa Russia Vladimir Putin ameunga mkono pendekezo la Marekani la kusitisha vita kati ya Russia na Ukraine lakini amesisitiza umuhimu wa kufanyia kazi maelezo yaliyomo katika pendekezo hilo.
Rais wa Marekani Donald Trump Jumatano kwenye Ikulu ya Marekani amekutana na Waziri Mkuu wa Ireland Michael Martin wakati wakifanya mazungumzo mapana kuanzia tofauti za kibiashara hadi mzozo wa Gaza, ingawa wote waliahidi kuimarisha ushirikiano kati ya nchi hizo mbili.
Vita vya kibiashara vya Marekani na Canada na Umoja wa Ulaya vilishika kasi Jumatano, huku Rais Donald Trump na washirika wa Marekani wakiwekeana ushuru mpya.
Mtaalam wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa nchini Haiti, William O’Neil Jumanne ameambia wanahabari mjini New York kwamba hali ya kiusalama nchini humo ni tete huku akisihi wahusika wa kitaifa na kimataifa kuheshimu haki za binadamu.
Maafisa wa Marekani na Ukraine walikutana Jumanne mjini Jeddah, Saudi Arabia kwa mazungumzo kuhusu juhudi za kumaliza vita kati ya Russia na Ukraine, huku pande zote mbili zikisema Kyiv inaunga mkono mpango wa Marekani wa sitisho la mapigano kwa siku 30.
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Marco Rubio Jumatatu alisema Marekani inatumai kutatua suala la misaada kwa Ukraine iliyositishwa katika mazungumzo ya Jumanne na maafisa wa Ukraine mjini Jeddah, Saudi Arabia.
Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Papa Francis, ambaye afya yake imeendelea kuimarika wakati akipokea matibabu kutokana na homa ya mapafu, Jumapili aliwashukuru madaktari pamoja na wahudumu wa afya, ingawa hakuweza kuongoza maombi ya Angelus kwa mara ya nne mfululizo.
Ripoti hiyo iliyotolewa Alhamisi na idara ya Umoja wa Mataifa kuhusu haki za wanawake na usawa wa jinsia imegundua kuwa karibu robo moja ya serikali kote duniani zimeripoti kuzorota kwa haki za wanawake mwaka jana.
Rais wa Marekani Donald Trump Alhamisi amethibitisha kwamba utawala wake unafanya mashauriano na kundi la Hamas ambalo limeorodheshwa na Marekani ni la kigaidi.
Rais wa Marekani Donald Trump Alhamisi amechelewesha kwa wiki nne ushuru mpya wa asilimia 25 kwenye bidhaa nyingi kutoka Mexico na Canada kwa mauzo yake kuja Marekani.
Iran imekamilisha miezi miwili ya mazoezi makali ya kijeshi katika miongo kadhaa huku ikijaribu kuzuia uwezekano wa mashambulizi kutoka kwa mahasimu wake Israel na Marekani, watafiti wa usalama wameiambia VOA.
Wakati viongozi wa Umoja wa Ulaya wakijiandaa kwa mazungumzo ya dharura kuhusu misaada ya kijeshi baada ya utawala wa Trump kusitisha msaada wake kwa Ukraine, wataalam kadhaa wa Russia wanasema kuwa Moscow inajitahidi kuvuruga mshikamano wa Magharibi.
Rais wa Marekani Donald Trump Jumatano amechelewesha kwa mwezi mmoja ushuru mpya wa asilimia 25 kwa magari kutoka Mexico na Canada wakati kukiwa na wasi wasi kwamba vita vya biashara na mataifa hayo jirani huenda vikawaumiza watengenezaji watatu wakubwa wa magari nchini Marekani.
Canada, Mexico na China Jumanne wote wamesema kwamba wataweka ushuru wa majibu kwenye bidhaa kutoka Marekani kufutia hatua ya Rais wa Marekani Donald Trump ya kuweka ushuru mpya kwa bidhaa zao zinazoingia Marekani.
Marekani imeweka bayana kwamba haitakuwa ikitoa mchango wa moja kwa moja kwa majukwaa ya Umoja wa Mataifa yakiwemo maendeleo endelevu pamoja na malengo mengine ya kimataifa ikijumuisha kutokomeza umaskini, katika upigaji kura kwenye Baraza Kuu la Umoja huo Jumanne.
Pandisha zaidi