Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 28, 2025 Local time: 06:38

Trump athibitisha kuhusu mashauriano na Hamas


Rais wa Marekani Donald Trump akiwa kwenye chumba cha Oval Office, kwenye Ikulu ya Marekani.
Rais wa Marekani Donald Trump akiwa kwenye chumba cha Oval Office, kwenye Ikulu ya Marekani.

Rais wa Marekani Donald Trump Alhamisi amethibitisha kwamba utawala wake unafanya mashauriano na kundi la Hamas ambalo limeorodheshwa na Marekani ni la kigaidi.

Hatua hiyo ni ili kushinikiza kuachiliwa kwa mateka waliobaki, akisisitiza onyo lake la awali kwamba watalipia gharama kubwa huko Gaza, iwapo hawatawaachilia mara moja. “Mtajua ninachosema,” Trump alisema akiwa kwenye chumba cha Oval, huko White House, baada ya kuulizwa na mwanahabari alichomaanisha.

Trump pia aliangazia mkutano wake wa Jumatano na baadhi ya mateka waliyoachiliwa. Mapema Alhamisi, mjumbe maalum wa Trump kwa Mashariki ya Kati Steve Witkoff aliwaambia wanahabari huko White House kwamba huenda hatua fulani zikachukuliwa na utawala wa Marekani kwa ushirikiano na Israel. Trump wala White House hawajasema iwapo hatua inayokusudiwa kuchukuliwa dhidi ya Hamas itakuwa ya kijeshi.

Forum

XS
SM
MD
LG