Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 28, 2025 Local time: 09:01

Trump achelewesha ushuru wa magari dhidi ya Canada na Mexico


Rais wa Marekani Donald Trump.
Rais wa Marekani Donald Trump.

Rais wa Marekani Donald Trump Jumatano amechelewesha kwa mwezi mmoja ushuru mpya wa asilimia 25 kwa magari kutoka Mexico na Canada wakati kukiwa na wasi wasi kwamba vita vya biashara na mataifa hayo jirani huenda vikawaumiza watengenezaji watatu wakubwa wa magari nchini Marekani.

Trump alizungumza na maafisa wa ngazi ya juu wa kampuni ya magari ya Ford, General Motors na Stellantis kabla ya kutangaza kuchelewesha, msemaji wa White House, Karoline Leavitt aliwaambia wanahabari.Alisema kwamba Trump aliwasihi watengeneza magari hao kuhamisha viwanda vyao kutoka Mexico na Canada hadi Marekani, ili kuepuka kulipa ushuru.

Hata hivyo ushuru mpya kwenye bidhaa nyingine kutoka Mexico na Canada bado upo, ingawa Leavitt alisema kuwa rais yuko tayari kwa mazungumzo ya kutafuta mbadala.Trump alitangaza uchelewesho wa ushuru wa magari baada ya kuongea awali na Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau ambapo kwa kwa mujibu wa Associated Press, Canada haipo tayari kuondoa ushuru iliyouweka kama Trump ataacha ushuru mwingine kwa Canada.

Forum

XS
SM
MD
LG