Rais Salva Kiir aliongoza sherehe za kuzinduliwa utaratibu ambao ni sehemu ya makubaliano ya amani yaliyofikiwa pamoja na mpinzani wake Rick Machar mwa 2018.
Taifa hilo changa kabisa duniani limekuwa likiongozwa na katiba za mpito wakati wa miaka ya vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyotokea baada ya uhuru hapo julai 2011.
Sudan ya Kusini ilitumbukia kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe Disemba 2013 baada ya Kiir kumtuhumu Machar kupanga njama ya kumpindua.
Ugomvi huo ambao ulioshuhudia ubakaji ukitumiwa kama silaha ya vita ulisababisha vifo vya zaidi ya watu 380,000 na kuwakosesha makazi watu wengine milioni 4.