Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Machi 19, 2024 Local time: 08:02

Saudi Arabia yatangaza utaratibu wa Ibada ya Hijja 2021


FILE - Julai 31, 2020, mahujaji wakizunguka Kaaba katika msikiti Mtukufu wa Makka, mjini Makka, Saudi Arabia.
FILE - Julai 31, 2020, mahujaji wakizunguka Kaaba katika msikiti Mtukufu wa Makka, mjini Makka, Saudi Arabia.

Saudi Arabia imetangaza Jumamosi kuwa Ibada ya Hijja mwaka 2021 imewekewa idadi isiyozidi watu elfu 60 wote hao wako ndani ya ufalme huo.

Uamuzi huu unatokana na kuendelea kwa janga la virusi vya corona.

Tangazo lilitolewa na ufalme huo linakuja baada ya hatua kama hiyo kuchukuliwa mwaka 2020 kuhusu Ibada ya Hijja kutokana na virusi, lakini bado iliruhusu idadi ndogo ya waumini kushiriki katika ibada hiyo.

Taarifa iliyotangazwa na shirika la habari la Saudi Arabia imekariri Wizara ya Hajj na Umrah kutoa tangazo hilo.

Kwa mujibu wa shirika la habari la Reuters taarifa imesema Ibada ya Hijja mwaka huu itaanza katikati ya mwezi Julai na itakuwa kwa watu wenye umri wa miaka 18 mpaka 65. Wale watakaoshiriki ibadah hii lazima wapatiwe chanjo, wizara imesema.

Chanzo cha Habari : Reuters

XS
SM
MD
LG