Alikuwa akijulikana kwa kuelezea vita vyake vya muda mrefu dhidi ya ugonjwa huo, mwandishi huyo wa vitabu, alilazwa hospitali siku ya Jumatatu kama sehemu ya matibabu yake aliyokuwa akiendelea nayo, msemaji wa familia alisema.
"Zoleka alifariki... akiwa amezungukwa na marafiki na familia," alisema Zwelabo Mandela.
Zoleka alikuwa mtoto wa binti wa mwisho wa Mandela, Zindzi Mandela, na mume wake wa kwanza, Zwelibanzi Hlongwane.
Familia hiyo ilisema uchunguzi wa hivi karibuni ulionyesha kusambaa "kwa kiasi kikubwa" kwa saratani ambayo iliathiri nyonga, ini, mapafu, ubongo na uti wa mgongo.
"Tunaomboleza kumpoteza mjukuu mpendwa wa mama Winnie na Madiba," Wakfu wa Nelson Mandela uliandika kwenye mitandao ya kijamii, ukitumia jina maarufu la mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel.
Chanzo cha habari hii ni shirika la habari la AFP.
Forum