Muungano wa kisiasa unaoongozwa na Waziri Mkuu wa India Narendra Modi, umeshinda viti vichache kwenye bunge, lakini changamoto kubwa kutoka kwa upinzani, imepunguza kwa kiasi kikubwa, ukubwa wa chama chake, na kuashiria kupungua kwa umaarufu wake baada ya muongo mmoja madarakani.