Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Januari 16, 2025 Local time: 07:33

Ahmadinejad ajiandikisha kuwania urais wa Iran


Rais wa zamani wa Iran Mahmoud Ahmadinejad akisamu wafuasi wake muda mfupi baada ya kujiandikisha kama mgombwa wa urais kwenye uchaguzi wa Juni 28.June 2, 2024.
Rais wa zamani wa Iran Mahmoud Ahmadinejad akisamu wafuasi wake muda mfupi baada ya kujiandikisha kama mgombwa wa urais kwenye uchaguzi wa Juni 28.June 2, 2024.

Rais wa zamani wa Iran mwenye msimamo mkali Mahmoud Ahmadinejad Jumapili amejiandikisha kuwania urais, ili kujaza nafasi ya rais Ibrahim Raisi iliyekufa hivi karibuni kutokana na ajali ya helikopta.

Hatua hiyo inatoa shinikizo kwa kiongozi mkuu wa taifa hilo Ayatollah Ali Khamenei, kwa kuwa alipokuwa ofisini, Ahmadinejad aliwahi kumkosoa wazi wazi, wakati juhudi zake za kuwania urais 2021 zilizuiliwa na mamlaka.

Kurejea kwa Ahmedinejad kwenye ulingo wa siasa kunakuja wakati kukiwa na mivutano kati ya Iran na mataifa ya Magharibi, kutokana na kuendelezwa kwa program ya nyuklia ya Tehran, kutoa silaha kwa Russia kwenye vita vyake dhidi ya Ukraine, pamoja na misako dhidi ya wakosoaji wake. Kufikia sasa Ahmadinejad ndiye mgombea mashuhuri kujiandikisha kuwania urais.

Akizungmmza muda mfupi baada ya kujiandikisha, ameapa kufanya mashauriano na dunia, wakati pia akiimarisha uhusiano wa kiuchumi na mataifa mengine, iwapo atashinda. Amesema kuwa ,”Matatizo ya kiuchumi, kisiasa, kitamaduni na kiusalama, yameongezeka kuliko ilivyokuwa 2013,” akiwa na maana ya mwaka ambao aliondoka madarakani.

Forum

XS
SM
MD
LG