Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Februari 09, 2025 Local time: 08:18

Maafisa wa afya wa Palestina wanasema shambulio la jeshi la Israel kwenye shule ya UN limeua watu 33


Watoto wa Kipalestina wakiruka kwenye vifusi vya jengo lililoharibiwa na shambulizi la anga la Israel kwenye kambi ya wakimbizi ya Nuseirat, katikati mwa Ukanda wa Gaza, Oktoba 30, 2023. Picha ya AFP
Watoto wa Kipalestina wakiruka kwenye vifusi vya jengo lililoharibiwa na shambulizi la anga la Israel kwenye kambi ya wakimbizi ya Nuseirat, katikati mwa Ukanda wa Gaza, Oktoba 30, 2023. Picha ya AFP

Jeshi la Israel Alhamisi lilifanya shambulizi la anga kwenye shule ya Umoja wa mataifa katikati mwa Gaza, ambako maafisa wa afya wa Palestina wamesema takriban watu 33 waliuawa.

Vikosi vya usalama vya Israel vilisema wapiganaji wa Hamas walioshiriki katika shambulio la Oktoba 7 dhidi ya Israel wamekuwa wakitumia shule hiyo kama makazi yao na “kuelekeza ugaidi” kutoka kwenye shule hiyo.

Ofisi ya vyombo vya habari ya Hamas imetupilia mbali taarifa ya Israel na kusema wanajeshi wa Israel walitekeleza “uhalifu wa kikatili” dhidi ya watu waliokoseshwa makazi yao na kusema wanawake na watoto ni miongoni mwa waliofariki.

Msemaji wa jeshi la Israel Luteni Kanali Peter Lerner aliwambia waandishi wa habari kwamba Israel haikuwa na taarifa kuhusu vifo vya raia.

Shambulio hilo lilitokea kwenye shule inayosimamiwa na shirika la Umoja wa mataifa linalohudumia wakimbizi wa Palestina huko Nuseirat.

Kamishna mkuu wa shirika hilo la misaada la Umoja wa mataifa Philippe Lazzarini, amelielezea tukio hilo kama “ siku nyingine ya ukatili huko Gaza.”

Forum

XS
SM
MD
LG