Waliokufa ni pamoja na mwanamke ambaye pikipiki yake iligongwa na mawe yaliyokuwa yanaporomoka, na kuharibu zaidi ya majengo 1,300, maafisa wamesema hivi leo Jumapili.
Tetemeko hilo halikusababisha tsunami. Idara ya Marekani ya jiolojia imesema kiwango cha tetemeko chenye ukubwa wa 6. katika kipimo cha rikta kimepiga kisiwa hicho cha pwani ya kusini saa nane mchana siku ya Jumamosi.
Kilikuwa katika eneo la kati ya kilometa 45 kusini mwa mji wa Sumberpucuung katika wilaya ya Malanga katika jimbo la Java Mashariki.
Rahmat Triyono, mkuu wa kituo cha tetemeko la ardhi na tsunami nchini Indonesia amesema mitetemo ya chini ya bahari haikusababisha tsunami.