Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 27, 2025 Local time: 12:40

Russia yachapisha picha ya kamanda wake aliyeuawa katika shambulio la Ukraine


Kamanda wa vikosi vya jeshi la majini katika bahari ya Black sea, Viktor Sokolov alipohudhuria hafla ya kuadhimisha miaka 240 ya vikosi hivyo huko Sevastopol, Crimea Mei 13, 2023. Picha na REUTERS/Alexey Pavlishak
Kamanda wa vikosi vya jeshi la majini katika bahari ya Black sea, Viktor Sokolov alipohudhuria hafla ya kuadhimisha miaka 240 ya vikosi hivyo huko Sevastopol, Crimea Mei 13, 2023. Picha na REUTERS/Alexey Pavlishak

Wizara ya Ulinzi ya Russia siku ya Jumanne ilichapisha picha zinazomuonyesha kamanda wa vikosi vya jeshi la majini katika bahari ya Black Sea, siku moja baada ya Ukraine kudai kuwa imemuua afisa huyo wa ngazi za juu katika shambulio la kombora.

Kyiv ilisema imewaua maafisa 34, akiwemo afisa wa ngazi ya juu wa jeshi la majini Viktor Sokolov, katika shambulizi ambalo halijawahi kutokea wiki iliyopita kwenye makao makuu ya jeshi la majnii katika peninsula ya Crimea inayokaliwa na Russia.

Sokolov, akiwa amevalia sare, alionyeshwa kwa njia ya video akishiriki mkutano uliokuwa ukiongozwa na waziri wa Ulinzi Sergei Shoigu.

Taarifa ya wizara ilisema mkutano huo ulifanyika siku hiyo asubuhi, lakini haikumtaja Sokolov.

Pia alionekana mara kadhaa kwenye picha ya video hiyo ya dakika nane iliyotolewa na wizara lakini Sokolov hakuonyeshwa akizungumza.

Kremlin iliwaambia waandishi wa habari muda mfupi kabla ya taarifa ya wizara hiyo kuwa "haina habari" kuhusu hali ya kamanda huyo na kuahirisha maswali kwa wizara ya ulinzi.

Jumanne jioni, vikosi maalum vya Ukraine vilisema "vilifafanua" maelezo kuhusu mashambulizi hayo ya wiki iliyopita.

“Wengi (maafisa waliouawa) bado hawajatambuliwa kwa sababu sehemu za miiili yao zimetawanyika,” walisema.

Shambulio hilo ni pigo kubwa kwa Moscow, ambayo imekumbwa na mashambulizi kadhaa kwenye bandari muhimu ya kimkakati ya Sevastopol katika miezi ya hivi karibuni.

Crimea ilichukuliwa na Russia mwaka 2014, na ni kitovu muhimu cha shughuli za jeshi la Moscow.

Chanzo cha habari ni shiriuka la habari la AFP

Forum

XS
SM
MD
LG