Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 18, 2024 Local time: 08:36

Rais wa zamani Kaunda alazwa hospitali Lusaka


Rais mstaafu wa Zambia Kenneth Kaunda
Rais mstaafu wa Zambia Kenneth Kaunda

Rais wa zamani wa Zambia Kenneth Kaunda mwenye umri wa miaka 97 anapewa matibabu ya ugonjwa ambao haukutajwa, kwenye hospitali ya kijeshi ya mjini Lusaka, ofisi yake imesema Jumatatu.

Kaunda aliiongoza Zambia tangu mwaka 1994 wakati taifa hilo la kusini mwa Afrika lilipojipatia uhuru, hadi mwaka 1991. Ni miongoni mwa mashujaa wachache walioshiriki kuikomboa Afrika ambaye bado yuko hai.

Msaidizi wake Rodrick Ngolo amesema katika taarifa kwamba Kaunda amekuwa hajisikii vizuri na amelazwa katika hospitali ya Maina Soko mjini Lusaka.

Taarifa ya Ngolo inasema “ mheshimiwa Kaunda anaomba wa Zambia wote na jumuia ya kimataifa kumuombea wakati timu ya madaktari inafanya kila kitu kuhakikisha anapona.”

Chanzo cha Habari : Reuters

XS
SM
MD
LG