Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 16:20

Mwanaharakati maarufu mtetezi wa wanawake atunukiwa tuzo ya haki za binadamu


 Amira Osman Hamed ,Khartoum, Sept. 8, 2013.
Amira Osman Hamed ,Khartoum, Sept. 8, 2013.

Amira Osman Hamed ni miongoni mwa washindi wa mwaka huu wa tuzo ya Front line defenders Award for Human Rights Defenders at Risk, shirikia hilo limetangaza Ijumaa.

Mwanaharakati huyo na mhandisi ambaye ana miaka 40 sasa amekuwa akiteteta haki za wanawake wa sudan kwa miongo miwili. kwa mujibu wa waandaaji wa tuzo hiyo, amekuwa muathirika wa ukiukwaji wa haki za wanawake na mwaka 2013 alikamatwa na kushitakiwa baada ya kukataa kuvaa hijabu inayovaliwa na wanawake wa kiislamu kufunika nywele zao.

Pia alishitakiwa mwaka 2002 kwa kuvaa suruali na mwezi January mwaka huu alichukuliwa kutoka kwenye nyumba yake na kushikiliwa mahali na maafisa wa usalama bila kuwa na mawasiliano kabla ya kuachiliwa baadae.

XS
SM
MD
LG