Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 15:59

Sudan yawaachilia huru wanaharakati waliopinga mapinduzi ya kijeshi


Kiongozi wa Baraza la uongozi wa mpito nchini Sudan akiwatizama raia na wanajeshi wajumbe wa Baraza hilo kuu wakila kiapo kwenye Ikulu, August 21, 2019. Picha ya Reuters.
Kiongozi wa Baraza la uongozi wa mpito nchini Sudan akiwatizama raia na wanajeshi wajumbe wa Baraza hilo kuu wakila kiapo kwenye Ikulu, August 21, 2019. Picha ya Reuters.

Sudan Jumatano imewaachilia huru viongozi kadhaa wa kiraia na mjumbe wa zamani wa Baraza kuu la uongozi, waliokamatwa katika miezi iliyofuata mapinduzi ya kijeshi mwaka jana, wakili wao amesema.

“Viongozi wote wa vuguvugu la the Forces for Freedom and Change, ambao walikuwa kizuizini katika wiki za karibuni, wameachiliwa,” wakili Azhari al-Haj ameiambia AFP.

The Forces for Freedom and Change (FFC), ni kundi kubwa la kiraia la Sudan lililoondolewa madarakani kufuatia mapinduzi ya kijeshi ya tarehe 25 Oktoba yaliyoongozwa na mkuu wa jeshi Abdel Fattah al-Burhan.

Mapinduzi hayo yalikwamisha mchakato wa kurejesha utawala wa kiraia ulioanzishwa baada ya kiongozi wa muda mrefu Omar al Bashir kuondolewa madarakani mwaka wa 2019.

Wajumbe wa FFC walioachiliwa huru ni pamoja na Babiker Faisal, Wagdi Saleh na Taha Othman, wakili wao amesema, vile vile mjumbe wa zamani wa Baraza kuu la uongozi, Mohamed al-Fekki.

Aliyekuwa waziri wa masuala ya baraza la mawaziri kabla ya mapinduzi Khaled Youssef, aliachiliwa Jumanne.

XS
SM
MD
LG