Baadhi ya watu waliokwama ambao walishindwa kutoka katika nyumba zao kwenye miji ya Sharjah na Fujairah waliokolewa na askari wa ulinzi wa raia.
Fujairah imeathiriwa vibaya kutokana na hali yake ya asili ya milima na miinuko.
Sharjah pia imeathiriwa wakati Dubai na Abu Dhabi zilishuhudia mvua kidogo.
Maafisa walitoa tahadhari ya mvua kwa wakazi kubaki nyumbani na kutofika maeneo ambayo yameelezwa kuwa na mafuriko kama vile mabonde.
Pia wametangaza makazi ya muda yatatolewa katika hoteli kwa wale watakaotakiwa kuondoka katika nyumba zao.
Hali ya hewa mbaya imeshuhudiwa nchini humo Jumatano ilitarajiwa kuendelea hivyo hadi leo alhamisi.