Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Januari 14, 2025 Local time: 10:36

Iran yakamilisha mipango ya kupokea ndege za kivita kutoka Russia


FILE PHOTO: Sukhoi Su-35 jet fighter drives along the airfield during International military-technical forum "Army-2020" at Kubinka airbase in Moscow Region
FILE PHOTO: Sukhoi Su-35 jet fighter drives along the airfield during International military-technical forum "Army-2020" at Kubinka airbase in Moscow Region

Iran imekamilisha mipango ya kupokea ndege za kivita za Russia aina ya Sukhoi SU-35 na helikopta kadhaa, naibu waziri wa ulinzi wa Iran ameliambia shirika la habari la Iran Tasnim Jumanne, wakati Tehran na Moscow zikiimarisha uhusiano  wa karibu wa kijeshi.

Mehdi Farahi
Mehdi Farahi

Jeshi la Iran la anga lina darzeni chache za ndege za kivita, ikiwemo ndege za kivita za Russia na zile kongwe za Kimarekani zilizo nunuliwa kabla ya Mapinduzi ya Kiislam ya mwaka 1979.

“Mipango imekamilika ya kupokea ndege za kivita aina ya Sukhoi Su-35, helikopta za mashambulizi aina ya Mil Mi-28, na ndege za mafunzo za kivita aina ya Yak-130 ambazo zitakuwa sehemu ya vikosi vya mashambulizi vya Jeshi la Iran,” naibu waziri wa ulinzi wa Iran Mehdi Farahi alisema.

FILE - Ndege za kivita aina ya Sukhoi Su-35
FILE - Ndege za kivita aina ya Sukhoi Su-35

Ripoti iliyotolewa na Tasnim haikujumuisha uthibitisho wowote kutoka Russia kuhusu makubaliano hayo.

Mwaka 2018, Iran ilisema imeanza kutengeneza aina ya ndege ya kivita iliyobuniwa nchini kwa ajili ya matumizi katika jeshi lake la anga.

Wataalam wa kijeshi wanaamini ndege hiyo ya kivita ni igizo la ndege aina ya F-5, ambayo ilitengenezwa hapo awali nchini Marekani katika miaka ya 1960.

Habari hii imetokana na shirika la habari la Reuters

Forum

XS
SM
MD
LG