Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Januari 24, 2025 Local time: 02:03

Vikosi vya Marekani vyashambuliwa Iraw na Syria


Vikosi vya Marekani vilishambuliwa mara nne Iraq, na Syria, Alhamisi kwa roketi na ndege zisizo na rubani, lakini hakukuwa na majeruhi au uharibifu wa miundombinu, afisa wa kijeshi wa Marekani amesema.

Akizungumza kwa masharti ya kutotajwa jina, amesema vikosi vya Marekani na kimataifa vilishambuliwa katika maeneo mawili kaskazini mashariki mwa Syria kwa roketi nyingi na ndege isiyo na rubani.

Nchini Iraq, ndege nyingi zisizo na rubani zilirushwa katika kituo cha anga cha Ain Al-Asad, magharibi mwa Baghdad na kuzinduliwa katika kambi ya wanajeshi wa Marekani karibu na uwanja wa ndege wa Irbil kaskazini mwa Iraq.

Kundi linalojiita Islamic Resistance la Iraq, ambalo wachambuzi wanasema ni mtego wa makundi kadhaa ya waasi ya Iraq yenye ushirikiano na Iran, lilidai kushambulia maeneo hayo mapema siku hiyo.

Forum

XS
SM
MD
LG