Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Aprili 28, 2025 Local time: 19:27

IAEA na Iran zakubaliana kuendeleza ukaguzi


Rais wa Iran Ebrahim Raisi akisalimiana na Rafael Grossi, mkuu wa shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki wakati wa kuanza mazungumzo katika ofisi ya Rais, Tehran, Machi 4, 2023. (Picha kwa hisani ya Ofisi ya Rais ya Iran kupitia shirika la habari la AP)
Rais wa Iran Ebrahim Raisi akisalimiana na Rafael Grossi, mkuu wa shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki wakati wa kuanza mazungumzo katika ofisi ya Rais, Tehran, Machi 4, 2023. (Picha kwa hisani ya Ofisi ya Rais ya Iran kupitia shirika la habari la AP)

Rafael Grossi, mkuu wa shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki, alisema Jumamosi wakati aliporejea kutoka katika ziara yake nchini  Iran kuwa Tehran imekubali kurejesha ‘baadhi ya ruhusa’ katika maeneo ya nyuklia na kuruhusu ukaguzi zaidi.

Iran imekuwa ikikwamisha makubaliano ambayo yatairuhusu IAEA kuchunguza vinu vyake ambako chembechembe za uranium ziligunduliwa. Iran pia imekubali kurejesha kamera na vifaa vingine vya ufuatiliaji ambavyo viliondolewa kutoka katika maeneno hayo.

IAEA na Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran zimetoa taarifa ya pamoja Jumamosi zikisema “mikutano ya ngazi ya juu” wakati wa ziara ya siku mbili ya Grossi “ilishughulikia umuhimu wa kuchukua hatua ili kuwezesha kuimarisha ushirikiano, kuharakisha inavyopaswa azimio la masuala ya udhibiti yaliyokuwa hayajakamilika.”

Taarifa hiyo ilisema mazungumzo kati ya IAEA na Iran “yatafanyika kwa moyo wa ushirikiano, na kwa kufuata kikamilifu muongozo wa IAEA na haki na majukumu ya Jamhuri ya Kiislam ya Iran, ikizingatia makubaliano kamili ya udhibiti huo.

Grossi alizungumza na waandishi Jumamosi huko Vienna. Akijibu swali la mwandishi wa VOA, Grossi alisema kuwa IAEA na shirika la Iran “wamekubaliana juu ya mambo mahsusi kadhaa” na kuwa IAEA itapewa “baadhi ya ruhusa” lakini haikuziorodhesha.

Alisema shirika lake “siku zote litakuwa wazi katika misingi ya mafanikio yake ambayo ana matumaini nayo.”

“Tunachukua hatua zenye mwelekeo sahihi,” Grossi alisema, “lakini sitaki kusikika kuwa na matumaini sana au kukata tamaa.”

“Nafikiri tuna kazi ngumu mbele yetu,” Grossi alisema, “kuna kazi nyingi mbele yetu kwa Iran na sisi wenyewe.

XS
SM
MD
LG