Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Mei 01, 2024 Local time: 12:29

DRC kutengeneza bidhaa zilizoongezwa thamani


Wachimbaji wadogowadogo wakichimba dhahabu eneo la Bukavu, DRC, tarehe 29 Machi , 2017.Picha na GRIFF TAPPER / AFP.
Wachimbaji wadogowadogo wakichimba dhahabu eneo la Bukavu, DRC, tarehe 29 Machi , 2017.Picha na GRIFF TAPPER / AFP.

Kampuni tanzu ya uchimbaji madini ya serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ya Gecamines ilisema Jumanne kwamba imepata dola milioni 75 za ufadhili wa kujenga kitengo kipya cha hydro-metallurgical cha kuzalisha vifaa vinavyotumika katika utengenezaji semiconductor.

Kampuni ya STL, inalenga kufanya matumizi ya kibiashara kwa kutumia madini huko Lubumbashi, mji mkuu wa mkoa wa Katanga wenye madini ulioko kusini mashariki mwa Kongo. alisema ufadhili huo mpya pia utaongeza muda wa vifaa vyake kwa miaka 30.

Kitengo kipya, kinatarajiwa kufanya kazi kuanzia mwezi Agosti mwaka huu , kitaanza kutengeneza kathodes za shaba, hidroksidi za kobalti, precipitate ya germanium, makinikia ya fedha na oksidi za zinki, STL alisema katika taarifa.

"Kwa mara ya kwanza, usindikaji wa aloi utakuwa iliyofanywa katika bara la Afrika ... na Waafrika, wakitengeneza bidhaa zilizoongezwa thamani," ilisema.

"STL pia itakuwa mhusika mkuu katika utengenezaji wa germanium duniani , chuma muhimu katika uzalishaji wa semiconductor."

Sehemu ya ufadhili mpya umetokana na fedha za kampuni hiyo, wakati banki ya Rawbank SA iliyoko nchini huko imetoa mkopo, STL ilisema.

Baadhi ya taarifa za habari hii inatoka katika shirika la habari la Reuters.

XS
SM
MD
LG