Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Desemba 13, 2025 Local time: 14:05

Watu kadhaa wafariki baada ya ndege ya Japan Airlines kugongana na nyingine ya walinzi wa pwani


Ndege katika Uwanja wa ndege wa Haneda mjini Tokyo, Japan
Ndege katika Uwanja wa ndege wa Haneda mjini Tokyo, Japan

Watu wasiopungua watano wamepoteza maisha yao baada ya ndege ya abiria ya Japan kushika moto Jumanne usiku wakati ikiteremka kwenye barabara ya uwanja wa ndege wa Haneda mjini Tokyo, baada ya kugongana na nyingine.

Duru za habari zinaarifu kuwa abiria na wafanyakazi wote walitolewa kwa ndege hiyo iliyokuwa ikichomeka.

Picha za televisheni zilionyesha miali ya moto ikitokea kwenye madirisha na sehemu ya ndani ya ndege ya shirika la ndege la Japan Airlines wakati wazima moto wakipambana na moto huo.

Vyombo vya habari vya Japan viliripoti kuwa ndege hiyo ilitua katika uwanja wa Haneda ikitokea kwa uwanja wa ndege wa Shin-Chitose huko Hokkaido, zaidi ya kilomita 1,200 kaskazini mwa Tokyo, ikiwa na abiria 379 na wafanyakazi.

Taarifa zilieleza kwamba ndege hiyo huenda iligongana na ndege ya walinzi wa pwani ya Japan.

Vyombo vya habari viliripoti kuwa wafanyakazi watano kati ya sita waliokuwa kwenye ndege ya walinzi wa pwani walithibitishwa kufariki.

Forum

XS
SM
MD
LG