Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Julai 27, 2024 Local time: 04:50

Matumaini ya kuwaokoa watu waliokwama chini ya kifusi Uturuki na Syria yafifia


Watu wajitolea misaada kwa maeneo yaliokumbwa na tetemeko huko katika mji wa Izmir, Uturuki.
Watu wajitolea misaada kwa maeneo yaliokumbwa na tetemeko huko katika mji wa Izmir, Uturuki.

Matumaini  ya kuwaokoa watu zaidi nchini Uturuki na Syria waliokwama chini aya vifusi  vya tetemeko la ardhi la 7.8 kwa kipimo cha rikta yanafifia.

Lakini siku ya Ijumaa - siku nne baada ya tetemeko hilo – manusura kadhaa walitolewa kutoka kwenye magofu katika jimbo la Hatay kusini mwa Uturuki, akiwemo mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka 10 na mama yake.

Maafisa wanasema idadi ya watu waliofariki kutokana na tetemeko kubwa la ardhi lililopiga mkoa wa mpakani kati ya Uturuki na Syria siku ya Jumatatu imefikia zaidi ya watu 21,000, na kufanya kuwa ni tetemeko baya zaidi la ardhi kuwahi kutokea tangu lile la tsunami la mwaka 2011 ambalo lililouwa takribani watu 20,000 nchini Japan.

Juhudi za vikosi vya uokoaji zinakwamishwa na ukosefu wa vifaa.

Waziri wa Ulinzi wa Uturuki Hulusi Akar akiongea na waandishi wa habari Ankara
Waziri wa Ulinzi wa Uturuki Hulusi Akar akiongea na waandishi wa habari Ankara

Mpaka Alhamisi, msafara wa malori sita ya msaada ya Umoja wa Mataifa kupitia kivuko cha Bab al-Hawa, kivuko pekee ambacho Umoja wa Mataifa umeidhinisha kutumika kupeleka misaada ya kibinadamu kutoka Uturuki kwenda kaskazini mwa Syria yameshindwa kufikia maeneo ambayo hayako chini ya utawala wa Syria.

Barabara inayoelekea kwenye kivuko upande wa Uturuki iliyoharibiwa na tetemeko hilo ilikuwa ndio kwanza limefunguliwa tena.

Maeneo ya utafutaji pia yamekuwa na sherehe kiasi watu wanapopatikana wakiwa hai na kupelekwa kupatiwa matibabu. Lakini kufukua vifusi pia kumemaanisha kuongezeka haraka kwa idadi ya vifo.

XS
SM
MD
LG