Erdogan ambaye atagombea uchaguzi wa mwezi Mei, amesema wakati wa ziara kwenye eneo kulikotokea janga hilo kwamba shughuli za uokoaji sasa zinafanyika kama kawaida na kuahidi kuwa hakuna mtu atakayeachwa bila makazi, huku idadi ya vifo vilivyoripotiwa kote Uturuki na nchi jirani ya Syria vikiongezeka na kufikia 12,000.
Katika eneo la kusini mwa Uturuki, watu walitafuta makazi ya muda na chakula katika hali ya hewa ya baridi kali, na kusubiri kwa uchungu kuona familia na marifiki zao ambao pengine bado wamezikwa chini ya lundo la vifusi.
Waokoaji wameendelea kuwapata baadhi ya watu wakiwa hai.
Lakini Waturuki wengi walilalamika juu ya ukosefu wa vifaa, utaalamu na msaada kuwaokoa wale waliokwama chini ya vifusi, wakati mwingine hata wakisikia vilio vyao, vya kuomba msaada.
Facebook Forum