Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 28, 2025 Local time: 16:05

Wawakilishi wa mkutano wa COP28 wakubaliana kupunguza mafuta ghafi


Wajumbe wa hali ya hewa kutoka Marekani John Kerry na Xie Zhenhua kutoka China wakiwa katika mkutano na waandishi wa habari. December 13, 2023. picha na REUTERS/Amr Alfiky
Wajumbe wa hali ya hewa kutoka Marekani John Kerry na Xie Zhenhua kutoka China wakiwa katika mkutano na waandishi wa habari. December 13, 2023. picha na REUTERS/Amr Alfiky

Wawakilishi kutoka karibu nchi 200 wamekubaliana katika Mkutano wa COP28 wa hali ya hewa hapo Jumanne kuanza kupunguza mafuta ghafi katika kukabiliana na hali ya hewa mbaya ikiwa ni makubaliano ya kwanza ya aina yake yanayoashiria mwisho wa enzi ya mafuta.

Makubaliano hayo yalifikiwa Dubai baada ya wiki mbili za mashauriano magumu ambayo yalitarajiwa kutuma ishara yenye nguvu kwa wawekezaji na watunga sera kwamba dunia inaungana katika lengo lake la kuachana na mafuta ghafi jambo ambalo wanasayansi wanasema ni tumaini bora la kupambana na janga la hali ya hewa.

Rais wa COP28 Sultan Al Jaber ameuita mpango huo kuwa ni wa kihistoria. lakini akaongeza kuwa mafanikio yake yatakuwa katika utekelezaji wake.

“wakati wa usiku na mapema asubuhi, tulifanya kazi kwa pamoja kufikia muafaka. Uraisualisikiliza, ulishiriki na kuongoza. Ninaahidi nitajitahidi sana na nitakuwa pamoja nanyi katika kila hatua. Na nyinyi, wafanyakazi wenzangu na marafiki, mmejitokeza haswa, mmeonyesha mnaweza kubadilika, na kueka maslahi ya pamoja mbele badala ya maslahi binafsi.” Alisema Rais hyo wa COP28.

Aliongeza kwa kusema “Tumekabiliana na hali halisi na tumeiweka dunia katika mwelekeo sahihi. Tumeipatia mpango thabiti wa utekelezaji ili kufikia kiwango cha 1.5. ni mpango unaoongozwa na sayansi. Ni mpango wa usawa ambao unakabiliana na uzalishaji , kuziba mwanya na kutekeleza , kufikiria upya ufadhili wa kimataifa na kuondoa hasara na uharibifu.

Zaidi ya nchi 100 zimekuwa zikifanya ushawishi mkubwa katika makubaliano ya COP28 ili kuondoa matumizi ya mafuta , gesi makaa ya mawe lakini zilipinga upinzani mkali kutoka kundi la wazalishaji mafuta linaloongozwa na Saudi Arabia OPEC ambalo lilisema kuwa ulimwengu unaweza kuondoa hewa chafu bila kuachana na mafuta.

Forum

XS
SM
MD
LG