Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Januari 22, 2025 Local time: 15:02

Matumanini ya kumalizika Jumanne kwa mkutano wa COP28 yadidimia


Waandamanaji nje ya ukumbi wa mkutano wa COP28. Decemba 12, 2023.
Waandamanaji nje ya ukumbi wa mkutano wa COP28. Decemba 12, 2023.

Matumaini ya kumalizika kwa mkutano wa hali ya hewa wa COP28 unaofanyikia Dubai yamedidimia Jumanne kutokana na mataifa kutofautiana kwenye masuala kadhaa.

Masuala yenye utata ni pamoja na makubaliano kuhusu matumizi ya mafuta ya ghafi, yanayotajwa kuwa sababu moja wapo ya kuongeza kiwango cha joto duniani. Wanaharakati mapema Jumanne wamekusanyika karibu na ukumbi wa mkutano, wakiendelea na malalamiko yao ya kutaka kusitishwa matumizi ya mafuta ghafi, ufadhili kamili wa umma, uungaji mkono wa kijinsia, pamoja na haki za biinadamu.

Mmoja wa watu walioandamana Sebastien Duyck kutoka kituo cha kimataifa cha sheria za kimazingira, amesema kwamba anatarajia kuwa mataifa yalioendelea yatatimiza ahadi zao za kutoa fedha kwa ajili ya utunzaji wa mazingira. Mazungmzo hayo yalitarajiwa kumalizika Jumanne, lakini mara nyingi huwa yanachukua muda mrefu kutokana na washiriki kutokubaliana.

Forum

XS
SM
MD
LG