Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 25, 2024 Local time: 11:05

Walioambukizwa Covid mara mbili wako hatarini ya kupata magonjwa mengine - Utafiti


Mgonjwa wa Covid 19.
Mgonjwa wa Covid 19.

Watu ambao wameambukizwa COVID-19 zaidi ya mara moja, wana uwezekano mara mbili au tatu zaidi, kuwa na matatizo mengi ya kiafya kuliko wale ambao wameambukizwa mara moja tu, ripoti ya utafiti mkubwa wa kwanza juu ya suala hilo ilisema Alhamisi.

Maambukizi mengi yameongezeka huku janga hilo likiendelea kusababisha maafa na virusi vikiendelea kubadilika na kuwa aina mpya, lakini athari za kiafya za muda mrefu za kuambukizwa tena hazijawa wazi.

Watafiti wa Marekani walisema utafiti wao mpya uliochapishwa katika jarida la "Tiba ya Asili" ulikuwa wa kwanza kuangalia jinsi kuambukizwa tena, kunaongeza hatari ya matatizo ya kiafya.

Watafiti walichambua rekodi za matibabu za watu milioni 5.8, katika hifadhi ya takwimu kitaifa ya Idara ya masuala ya wazee ya Marekani.

Wakati watafiti walilinganisha matokeo ya kiafya ya vikundi tofauti, waligundua kuwa "watu walioambukizwa tena wana hatari kubwa ya matatizo ya kiafya," Ziyad Al-Aly, mtaalam wa magonjwa ya magonjwa katika Chuo Kikuu cha Washington huko St Louis na mkuu wa utafiti , aliliambia shirika la habari la AFP.

Watu walio na maambukizi ya kurudia walikuwa na uwezekano wa kufa kabla ya wakati na mara tatu zaidi ya uwezekano wa kulazwa hospitalini na ugonjwa kuliko wale ambao hawakuwa wameambukizwa tena, utafiti uligundua.

XS
SM
MD
LG