Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Machi 19, 2024 Local time: 12:21

Viongozi wa Afrika kuhudhuria mkutano maalum Addis Ababa


Makao Makuu ya Umoja wa Afrika, Addis Ababa, Ethiopia.
Makao Makuu ya Umoja wa Afrika, Addis Ababa, Ethiopia.

Viongozi  wa  Afrika wanatarajiwa kuanza kuwasili mjini Addis Ababa wikendi hii kuhudhuria mkutano  maalum wenye  lengo  la  kupitisha mageuzi  yaliyokuwa yakijadiliwa  kwa  muda  mrefu  katika  Umoja  huo  wa Afrika.

Mkutano huo maalum utafanyika katika makao makuu wa Umoja huo mjini Addis Ababa Jumamosi na Jumapili kwa msisitizo wa rais wa Rwanda Paul Kagame, ambaye amekuwa akiongoza shinikizo kuhusu mageuzi hayo.

Mabadiliko yanalenga kuuboresha na kuuwezesha Umoja wa Afrika - ambao ni wito wenye nguvu kwa muungano huo, ambao mara nyingi unaonekana kuwa usiyo na uwezo na unaotegemea zaidi wafadhili, na wadadisi wanasema muda wa kupatikana makubaliano ni mfupi.

Rais wa Rwanda, Paul Kagame.
Rais wa Rwanda, Paul Kagame.

Misri inatarajiwa kuchukua usukani mapema mwaka ujao, na wachambuzi wansema haionekani ikiwa na nia ya kuunga mkono mageuzi kwenye umoja huo.

Afrika Kusini, Zimbabwe, Botwana, Comoro, Togo na Ghana zimethibitisha kwamba zitawakilishwa na marais wao.

XS
SM
MD
LG