Rais wa Ukraine aondolewa madarakani na bunge huku wananchi wachukua udhibiti wa ikulu na afisi zote za serikali.
Waandamanaji wa upinzani wachukua udhibiti wa ikulu Ukraine

1
Kiongozi wa upinzani wa Ukraine Yulia Tymoshenko (Katikati) akisafirishwa kwenye kiti cha walemavu akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kiev baada ya kuachiliwa huru, Feb. 22, 2014.

2
Polisi wa kikosi maalum cha kupambana na ghasia cha Berkut, wanajitayarisha kuondoka kutoka kambi yao mjini Kiev. wakuu wa idara nne za usalama za Ukraine pamoja na kikosi cha Berkut walikwenda bungeni Jumamosi na kutangaza kwamba hawatopambana tena na wananchi. .

3
Wapinzani wa serikali wasimama zamu wakilinda bunge la taifa mjini Kiev, siku ya Jumamosi baada ya rais na serikali yake kuondolewa madarakani.

4
Yevgenia Tymoshenko (kulia) akilia kutokana na furaha nyingie pale Bunge lilipopiga kura kuachiliwa kwa mamake, kiongozi wa upinzani Yulia Tymoshenko, wakati wa kikao maalum Jumamosi mjini Kyiv. Feb, 22 2014.