Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Julai 11, 2025 Local time: 22:28

Tetemeko jipya lenye ukubwa wa 6.3 lalitikisa eneo la magharibi ya Afghanistan


Wakazi wa Afghanistan wakiondoa kifusi huku kutafuta miili ya waliouawa katika tetemeko la ardhi huko katika kijiji cha Kashkak, wilaya ya Zendeh Jan katika Jimbo la Herat, Octoba 8, 2023.
Wakazi wa Afghanistan wakiondoa kifusi huku kutafuta miili ya waliouawa katika tetemeko la ardhi huko katika kijiji cha Kashkak, wilaya ya Zendeh Jan katika Jimbo la Herat, Octoba 8, 2023.

Tetemeko jingine kubwa la ardhi limepiga Afghanistan leo Jumatano ambapo la awali liliua  watu zaidi ya 2,000 Jumamosi.

Tetemeko hilo la kiwango cha 6.8 kwa kipimo cha rikta lilikuwa takriban kilomita 28 nje ya Herat, mji mkuu wa jimbo la Herat.

Kitovu cha tetemeko la Jumamosi lilikuwa maili 25 kaskazini magharibi mwa mji huo, na matetemeko mengine baada ya hapo yalifuatia.

Maafisa wa Taliban wamesema zaidi ya watu 2,000 wamekufa huko Herat baada ya matetemeko ya awali.

Kundi la misaada la madaktari wasio na mipaka limesema hospitali ya kanda ya Herat imepokea watu 117 waliojeruhiwa kutokana na tetemeko la leo.

Tetemeko la leo pia limeharibu nyumba 700 katika kijiji cha Chahak ambacho kilikuwa hakijawahi kukumbwa na tetemeko katika siku zilizopita.

Forum

XS
SM
MD
LG