Siku mbili baada ya tetemeko kubwa la ardhi na mitetemeko mingi iliyofuata na kuua mamia ya watu na kujeruhi wengine wengi.
Tetemeko hilo la kipimo cha 6.3 lilitokea katika mkoa wa magharibi wa Herat, Jumamosi, na kuharibu zaidi ya vijiji kumi na mbili ndani na karibu ya wilaya ya Zinda Jan iliyoathirika zaidi. '
Maafisa na mashahidi walisema eneo la maafa lilitikiswa mara mbili na mitetemeko mipya Jumatatu, na kuukumba mji mkuu wa jimbo hilo, Herat, na kuwakimbiza maelfu ya wakaazi wake mitaani.
Wakati serikali ya Taliban imeripoti vifo vya takriban watu 2,000 tangu siku ya kwanza ya maafa Jumamosi, Umoja wa Mataifa umethibitisha vifo vya zaidi ya watu 1,000, na kusema kuwa karibu 1,700 walijeruhiwa.
Forum