Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Januari 14, 2025 Local time: 09:05

Idadi ya vifo katika tetemeko Afghanistan yapita 2,400


Idadi ya watu waliofariki katika tetemeko la ardhi la Jumamosi la kipimo cha 6.3, Afghanistan imepita 2,400 huku timu za utafutaji na uokoaji zikiondoa miili zaidi kwenye magofu ya mamia ya nyumba zilizoharibiwa, kwa mujibu wa maafisa wa mkoa huo.

“Baadhi tuna imani bado wapo chini ya vifusi,” alisema Matiul Haq Khalis, rais wa hilali nyekundu ya Afghanistan, baada ya kutembelea maeneo yaliyoathiriwa na tetemeko katika mkoa wa Herat, Jumanne.

Katika kijiji kilichopo katika kitovu cha tetemeko la ardhi, inaripotiwa kuwa takriban mauti 300 wamezikwa.

Wizara ya afya ya Afghanistan, imeripoti vifo 2,445 mpaka sasa, lakini ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu masuala ya kibinadamu (OCHA) imetoa idadi ndogo ya vifo kuwa ni 1,300 na watu 500 hawajulikani walipo.

Forum

XS
SM
MD
LG