Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Januari 22, 2025 Local time: 14:19

Afghanistan: Idadi ya waliofariki kutokana na tetemeko la ardhi yafikia 2,000


Afghanistan Earthquake
Afghanistan Earthquake

Idadi ya vifo kutokana na mfululizo wa matetemeko ya ardhi magharibi mwa Afghanistan iliongezeka haraka Jumapili hadi kufikia zaidi ya 2,000, serikali ya Taliban ilisema, huku miili ikiendelea kutolewa kutoka kwa vijiji vilivyobomolewa na kuzikwa kwenye makaburi ya jumla.

Zaidi ya nyumba 1,300 ziliporomoka wakati tetemeko la Jumamosi la kipimo cha 6.3 cha rikta-- likifuatiwa na mitetemeko minane mikubwa -- iliyotikisa maeneo ambayo ni magumu kufikia, takriban kilomita 30 kaskazini magharibi mwa mji mkuu wa mkoa wa Herat, kulingana na maafisa.

Katika wilaya ya vijijini ya Zinda Jan, kaya za vijiji zrundo la mawe na vifusi, ambapo timu za uokoaji za muda ziliendelea kuchimba katika juhudi za kuokoa watu na kuopoa mili siku ya Jumapili.

Misaada ilipelekwa taratibu katika eneo la janga hilo ikiwa ni pamoja na chakula, maji, mahema na majeneza.

Msemaji wa wizara ya usimamizi wa majanga Mullah Janan Sayeq alisema taifa hilo "lilishuhudia tetemeko la ardhi ambalo halijawahi kutokea," na kupelekea idadi ya waliofariki kuwa 2,053 katika vijiji 13 siku ya Jumapili.

Forum

XS
SM
MD
LG