Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Machi 22, 2025 Local time: 08:12

Watu 15 wafariki katika tetemeko la ardhi nchini Afghanistan


Ramani ya Afghanistan
Ramani ya Afghanistan

Watu 15 walifariki na wengine 40 kujeruhiwa katika mitetemeko kadhaa ya ardhi iliyopiga eneo la magharibi mwa Afghanistan leo Jumamosi, afisa wa usimamizi wa majanga ameliambia shirika la habari la Reuters.

Tetemeko hilo lilikuwa na ukubwa 6.3 kwenye vipimo vya rikta, taasisi ya Marekani ya utafiti wa kijeolojia ilisema, huku mitetemeko iliyofuata ikipiga kilomita 35 kaskazini magharibi mwa mji wa Herat.

Takwimu hizo za vifo ni za ripoti ya awali kutoka wilaya ya Zinda Jan ya jimbo la Herat, msemaji wa wizara ya usimamizi wa majanga Jan Sayeq alisema.

Aliongeza kuwa mitetemeko hiyo ilitikisa pia majimbo ya Farah na Badghis, ambako kumeripotiwa uharibifu mkubwa wa nyumba, lakini hakuna maelezo yaliyotolewa kuhusu vifo.

Forum

XS
SM
MD
LG