Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Desemba 04, 2023 Local time: 05:15

Taliban waharibu kituo cha Islamic State Kabul, waua wanamgambo wote


Mlinzi wa Taliban akilinda eneo lililotokea mlipuko Jumapili Kabul, Afghanistan Octoba 4, 2021. REUTERS/Staff
Mlinzi wa Taliban akilinda eneo lililotokea mlipuko Jumapili Kabul, Afghanistan Octoba 4, 2021. REUTERS/Staff

Chama tawala nchini Afghanistan cha Taliban kimesema Jumatatu vikosi vyake vya usalama viliharibu kituo cha Islamic State Khorasan mjini Kabul na kuwauwa wanamgambo wote.

Uvamizi huo wa usiku kucha ulikuja saa kadhaa baada ya shambulizi la bomu nje ya msikiti mkuu wa Eid Gah Jumapili na kuua raia wa Afghanistan wasiopungua wanane, na kuwajeruhi wengine 20.

Hata hivyo hakuna aliyedai kuhusika na shambulizi hilo la kwenye msikiti.

Taliban hawakusema operesheni yao dhidi ya kikundi cha Afghanistan chenye mahusiano na Islamic State maarufu kama ISIS-K ilikuwa majibu ya mlipuko wa bomu uliosababisha vifo kwenye msikiti.

Kituo cha Daesh kiliharibiwa kabisa na wanachama wote wa Daesh waliokuwa ndani waliuawa kutokana na matokeo ya operesheni yenye mafanikio iliyofanywa vikosi maalum vya Taliban, Zabihullah Mujahid, msemaji mkuu wa Taliban alitangaza mapema leo.

XS
SM
MD
LG