Wa-Catalan, wakazi wa jimbo la kaskazini la Hispania Catalonia walipiga kura Jumapili katika kura ya maoni ya kudai uhuru iliyopigwa marufuku na serikali ya Madrid. Polisi walijaribu kunyakua karatsi za kupiga kura katika angalau kituo kimoja . Mahakama ya Katiba ya Hispania iliahirisha upigaji kura na serikali kusema si halali lakini watu walijitokeza kupiga kura.
Wakazi wa Catalonia wapiga kura kudai uhuru
Licha ya serikali ya Hispania kupiga marufuku kura ya maoni ya kudai uhuru wa jimbo la kaskazini la Catlonia, lakini wapiga kura walijitokeza kwa wingi kushiriki huku katika maeneo mengi walipambana na polisi.

1
Mwanamke akipiga busu cheti ya kupiga kura kabla ya kuitia kwenye sanduku kwenye kituo cha kupiga kura kudai uhuru wa jimbo la Catalonia mjini Barcelona, Spain, Oct. 1, 2017.

2
Watu wakisukumana na polisi wa taifa walokua wanajaribu kuwazuia wafuasi wanaounga mkono kura ya maoni nje shule ya Ramon Llull iliyopangwa na serikali ya Catalana mjini Barzelona kua ni kituo cha kupiga kura, Oct.1, 2017.

3
Wapiga kura wakifurahia kupiga kura zao katika shule iliyopangwa kua kituo cha kupiga kura na serikali ya Catalan mtaa wa Gracia mjini Barcelona, Spain, Oct. 1, 2017.

4
Polisi wa kupambana na ghasia wakifyetua risasi za mpira dhidi ya watu walojaribu kukaribia kituo cha kupiga kura kushiriki katika kura ya maoni mjini Barcelona, Oct. 1, 2017.