Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 28, 2025 Local time: 09:15

Rwanda yadai DRC inapanga shambulizi 'kubwa' dhidi yake


Rais wa Rwanda Paul Kagame. Picha na Mariam KONE / AFP
Rais wa Rwanda Paul Kagame. Picha na Mariam KONE / AFP

Rwanda ilisema Ijumaa kwamba ina ushahidi wa mpango wa  Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kufanya  shambulizi dhidi yake, na kukanusha kuwa ilikuwa ikichochea migogoro ndani ya mpaka wa nchi hiyo, jirani yake.

Kigali na Kinshasa zimekuwa zikilaumiana kwa kuzuka upya kwa mapigano na ukosefu wa utulivu mashariki mwa Kongo, ambapo waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda wameuteka mji mkuu wa eneo hilo na wanasonga mbele katika maeneo zaidi, huku mamia wakiuawa na maelfu kufurushwa makwao

"Tunapinga vikali shuruma za DRC dhidi ya Rwanda kwa kuhusika katika kusababisha ukosefu wa utulivu mashariki mwa DRC," mwakilishi wa Rwanda katika Umoja wa Mataifa mjini Geneva, Uswizi, James Ngango, aliambia mkutano wa dharura wa Baraza la Haki za Kibinadamu.

"Kilicho wazi, hata hivyo, ni tishio kwa Rwanda linalosababishwa na hali inayoendelea hivi sasa. Kufuatia kuanguka kwa Goma, ushahidi mpya umepatikana kuhusiana na shambulio kubwa linalopangwa dhidi ya Rwanda," alisema na kuongeza kuwa Kinshasa na washirika wake walikuwa wamehifadhi silaha ndani na karibu na uwanja wa ndege wa Goma. Hadi tulipokuwa tukiandaa ripoti hii, hakukuwa na majibu ya moja kwa moja kutoka kwa maafisa wa serikali ya DRC.

Forum

XS
SM
MD
LG