Chama hicho cha wafanyakazi kwa jina NAPSAWU kimesema kwamba wanachama wake 50 walipelekwa hospitalini kwenye mji mkuu wa Mbabane huku wengine 30 wakipelekwa kwenye mji wa Manzini.
Kwa mujibu wa shirika la habari la AFP, mamia ya wanajeshi na polisi wanasemekana kufanya misako kwenye miji hiyo miwili wakati wakirusha gesi ya kutoa machozi pamoja na risasi za mipira kwa vikundi vya watu vilivyo kusanyika. Serikali pia inasemekana kufunga huduma za internet baada ya picha na video za ghasia kuanza kusambaa kwenye mitandao ya kijamii.
Nkambule ameambia AFP kwamba ghasia zilianza saa moja ya asubuhi wakati akilaumu maafisa wa usalama kwa kurusha gesi ya kutoa machozi kwenye basi lililobeba wafanyakazi waliokuwa wakiandamana. Baadhi ya video zilizosambazwa zinaonyesha baadhi ya watu wakiruka kutoka kwenye madirisha ya basi hilo likiwa limezingirwa na moshi mweupe.