Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Julai 27, 2024 Local time: 04:10

Rais wa Uturuki afanya ziara ya siku mbili Nigeria


Rais wa Uturuki apokelewa kwa shangwe Nigeria
please wait

No media source currently available

0:00 0:00:54 0:00

Rais wa Uturuki apokelewa kwa shangwe Nigeria

Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari amemkaribisha Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan nchini kwake Jumatano.

Erdowan atakuwa katika taifa hilo maarufu katika bara la Afrika kwa ziara ya siku mbili ya kikazi.

Kiongozi huyo wa Uturuki anasindikizwa na mkewe Emine Erdowan.

Katika taarifa msemaji wa Rais Shehu Garba alieleza Jumanne usiku kwamba Erdowan anatokea Angola na kuelekea Togo.

Buhari na mgeni wake watajadiliana kuhusu makubaliano dazeni mbili ya mikataba ya pande mbili na ushirikiano ambapo pia watapitisha baadhi kwa kusainiwa.

Taarifa zinasema baadae Erdowan atafanya mkutano wa faragha na Buhari.

Anatarajiwa kutembelea Kituo cha Utamaduni cha Uturuki katika mji wa Abuja wakati mkewe Emine na mwenzake wa Nigeria watatatembelea shule ya sekondari ya serikali iliyokarabatiwa huko Wuse 11.

EU calls o

XS
SM
MD
LG