Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Mei 02, 2024 Local time: 00:57

Mzozo kuhusu chanjo za Covid-19 waongezeka Marekani


Rais wa Marekani Joe Biden akizungumza na wanahabari kwenye ikulu mapema mwaka huu.
Rais wa Marekani Joe Biden akizungumza na wanahabari kwenye ikulu mapema mwaka huu.

Mzozo kuhusiana na utoaji wa chanjo za corona Marekani, huenda ukaongezeka katika wiki zijazo wakati amri mpya inayohitaji watu kuchukua kwa lazima ikikaribia kuanza kufanya kazi. 

Maafisa wa ikulu ya Marekani wanaendelea kukarabati amri ya rais Joe Biden, kwamba takriban wafanyakazi milioni 80 kwenye sekta ya biashara wapatiwe chanjo ili kuendelea kufanya kazi au wawe wakipimwa mara kwa mara iwapo wapo kwenye makampuni yenye zaidi ya wafanyakazi 100.

Hatua hiyo inawahitaji wafanyakazi wote wa serikali pamoja na wanajeshi kupokea chanjo hiyo kabla ya mwaka kumalizika. Ingawa wengi wa wanajeshi wa majini wa Marekani tayari wamepokea chanjo, baadhi ya maafisa wameanza kuwafukuza wale waliokataa.

Wakati huo huo, baadhi ya makampuni makubwa pamoja na mashirika yameanza kuwafukuza kazi wale waliokataa kupokea chanjo licha ya kwamba tayari wamarekani milioni 177 wamepokea chanjo hiyo ikiwemo thuluthi mbili ya watu wazima hapa nchini.

Baadhi ya wanajeshi wameanza kuweka video zao kwenye mitandao wakieleza masaibu wanayopitia kutokana na kukataa kupokea chanjo hiyo. Baadhi wanadai kwamba haki zao za kimsingi za kufanya maamuzi ya kiafya zinahujumiwa.

XS
SM
MD
LG