Vuguvugu hilo ambalo kwa wakati mmoja lilionekana kuwa na nguvu mno, lilishinda uchaguzi wa kwanza, huru, wa rais, nchini Misri mnamo mwaka wa 2012, lakini lilipinduliwa na jeshi mwaka mmoja baadaye, kufuatia maandamano makubwa ya kupinga utawala wake, na limevumilia ukandamizaji mkali wa mamlaka tangu wakati huo, kwa mujibu wa shirika la habari la Reuters.
Viongozi wake wengi na maelfu ya wafuasi wake, wako jela au wametoroka Misri, na kundi hilo limeondolewa kwenye mazungumzo ya kisiasa yatakayozinduliwa hivi karibuni na Rais Abdel Fattah al-Sisi, ambaye kama mkuu wa jeshi, aliondoa utawala wa vuguvugu hilo mnamo mwaka mwaka wa 2013.
Cairo imeliorodhesha kundi la Brotherhood kama shirika la kigaidi, lakini kaimu kiongozi Ibrahim. Munir, alisisitiza madai yamuda mrefu ya kundi hilo, kwamba linapinga ghasia.
Facebook Forum